Biblia ya King James Version
Yohana, Sura ya 16:
- Hayo nimewaambia, msije mkachukizwa.
- Watawatoa ninyi katika masinagogi; naam, wakati unakuja ambapo kila mtu akiwaua atadhani kwamba anamtumikia Mungu.
- Na haya watawatendea ninyi, kwa sababu hawakumjua Baba wala mimi.
- Lakini nimewaambieni mambo haya, ili wakati ule utakapofika, mkumbuke kwamba naliwaambieni hayo. Na mambo hayo sikuwaambia hapo mwanzo, kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
- Lakini sasa naenda zangu kwake yeye aliyenipeleka; wala hakuna hata mmoja wenu aniulizaye, Unakwenda wapi?
- Lakini kwa sababu nimewaambia hayo huzuni imejaa mioyoni mwenu.
- Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke; kwa maana nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; lakini nikienda zangu, nitampeleka kwenu.
- Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu;
- kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi;
- kwa habari ya haki, kwa sababu mimi naenda kwa Baba, nanyi hamnioni tena;
- kwa habari ya hukumu, kwa sababu mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa.
- Bado ningali ninayo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili sasa hivi.
- Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.
- Yeye atanitukuza mimi, kwa kuwa atatwaa katika yangu na kuwapasha habari.
- Yote aliyo nayo Baba ni yangu; kwa hiyo nalisema ya kwamba atatwaa katika yangu na kuwapasha habari.
- Bado kitambo kidogo nanyi hamnioni; na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona, kwa kuwa naenda kwa Baba.
- Basi baadhi ya wanafunzi wake wakasemezana, Ni nini hii anayotuambia, Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona; ?
- Basi wakasema, Ni nini hii asemayo, Bado kitambo kidogo? hatuwezi kusema anachosema.
- Yesu akajua ya kuwa walitaka kumwuliza, akawaambia, Je! mnaulizana ya kuwa nalisema, Bado kitambo kidogo nanyi hamnioni;
- Amin, amin, nawaambia, Ninyi mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utafurahi;
- Mwanamke akiwa katika utungu wa kuzaa huwa na huzuni kwa sababu saa yake imefika;
- Na ninyi sasa mna huzuni, lakini nitawaona tena, na mioyo yenu itafurahi, na furaha yenu hakuna awaondoleaye.
- Na siku hiyo hamtaniuliza neno lolote. Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu.
- Hata sasa hamkuomba neno kwa jina langu; ombeni, nanyi mtapata; furaha yenu iwe timilifu.
- Hayo nimewaambia kwa mithali, lakini wakati unakuja ambapo sitasema nanyi tena kwa mithali, bali nitawaonyesha waziwazi juu ya Baba.
- Siku ile mtaomba kwa jina langu, wala siwaambii ya kwamba nitawaombea kwa Baba;
- Kwa maana Baba mwenyewe anawapenda ninyi kwa sababu ninyi mmenipenda mimi na kuamini kwamba mimi nalitoka kwa Mungu.
- Nilitoka kwa Baba, na nimekuja ulimwenguni; tena nauacha ulimwengu, na kwenda kwa Baba.
- Wanafunzi wake wakamwambia, Tazama, sasa wanena waziwazi, wala husemi mithali.
- Sasa tunajua kwamba wewe unajua kila kitu, na huna haja ya mtu yeyote kukuuliza. Kwa hiyo tunaamini kwamba ulitoka kwa Mungu.
- Yesu akawajibu, Je!
- Tazama, saa inakuja, naam, imekwisha kuja, ambapo mtatawanywa, kila mtu kwao kwao, na kuniacha mimi peke yangu;
- Hayo nimewaambia mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mtapata dhiki, lakini jipeni moyo; nimeushinda ulimwengu.