Biblia ya King James Version
Yohana, Sura ya 14:
- Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi.
- Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia. naenda kuwaandalia mahali.
- Nami nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo.
- Na mimi niendako mwajua, na njia mnaijua.
- Tomaso akamwambia, Bwana, sisi hatujui uendako; na jinsi gani tunaweza kujua njia?
- Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
- Kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba yangu;
- Filipo akamwambia, Bwana, tuonyeshe Baba, na yatutosha.
- Yesu akamwambia, Mimi nimekuwa pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? yeye aliyeniona mimi amemwona Baba; nawe wasemaje basi, Utuonyeshe Baba?
- Husadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu? Maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa nafsi yangu;
- Mnisadiki ya kuwa mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu;
- Amin, amin, nawaambia, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi yeye naye atazifanya; na kubwa kuliko hizo atafanya; kwa sababu mimi naenda kwa Baba yangu.
- Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana.
- Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya.
- Mkinipenda, mtazishika amri zangu.
- Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele;
- Hata Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa sababu haumwoni wala haumtambui; kwa maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu.
- Sitawaacha ninyi yatima, nitakuja kwenu.
- Bado kitambo kidogo na ulimwengu hautaniona tena; lakini ninyi mnaniona, kwa kuwa mimi ni hai, ninyi nanyi mtakuwa hai.
- Siku ile mtajua ya kuwa mimi niko ndani ya Baba yangu, nanyi ndani yangu, nami ndani yenu.
- Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye; naye anipendaye atapendwa na Baba yangu, nami nitampenda na kujidhihirisha kwake.
- Yuda, siye Iskarioti, akamwambia, Bwana, imekuwaje ya kwamba wataka kujidhihirisha kwetu, wala si kwa ulimwengu?
- Yesu akajibu, akamwambia, Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda, nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake.
- Yeye asiyenipenda, yeye hayashiki maneno yangu, na neno hilo mnalolisikia si langu, bali ni la Baba aliyenituma.
- Hayo nimewaambia nikiwa bado nipo pamoja nanyi.
- Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.
- Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi si kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiogope.
- Mmesikia jinsi nilivyowaambia, naenda zangu, tena naja kwenu. Kama mngalinipenda, mngalifurahi kwa sababu nimesema, naenda kwa Baba, kwa maana Baba yangu ni mkuu kuliko mimi.
- Na sasa nimewaambia kabla halijatokea, ili litakapotokea mpate kuamini.
- Sitasema nanyi maneno mengi baadaye, kwa maana yuaja mkuu wa ulimwengu huu, wala hana kitu kwangu.
- Lakini ili ulimwengu ujue kwamba nampenda Baba; na kama vile Baba alivyoniamuru, ndivyo nifanyavyo. Ondokeni, twende zetu.