Basi Wayahudi wakasema, Tazama jinsi alivyompenda!
Na baadhi yao wakasema, Je!
Basi Yesu akiugua tena ndani yake akafika kaburini. Lilikuwa ni pango, na jiwe limewekwa juu yake.
Yesu akasema, Ondoeni jiwe. Martha, dada yake huyo aliyekufa, akamwambia, Bwana, amekwishaanza kunuka, kwa maana amekuwa maiti siku nne.
Yesu akamwambia, Mimi sikukuambia ya kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu?
Kisha wakaliondoa lile jiwe kutoka mahali alipolazwa maiti. Yesu akainua macho yake juu, akasema, Baba, nakushukuru kwa kuwa umenisikia.
Nami nilijua ya kuwa wewe wanisikia sikuzote;
Naye akiisha kusema hayo, akalia kwa sauti kuu, Lazaro, njoo huku nje.
Akatoka nje yule aliyekufa, amefungwa sanda miguuni na mikononi, na uso wake umefungwa kwa leso. Yesu akawaambia, Mfungueni, mkamwache aende zake.
Basi wengi katika Wayahudi waliokuja kwa Mariamu, na kuyaona aliyoyafanya Yesu, wakamwamini.
Lakini baadhi yao wakaenda kwa Mafarisayo, wakawaambia mambo aliyoyafanya Yesu.
Basi wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakakusanya baraza, wakasema, Tufanye nini? maana mtu huyu anafanya miujiza mingi.
Tukimwacha hivi, watu wote watamwamini; na Warumi watakuja na kuchukua mahali petu na taifa letu.
Mmoja wao, aitwaye Kayafa, aliyekuwa Kuhani Mkuu mwaka huo huo, akawaambia, Ninyi hamjui neno lo lote;
wala hatuoni ya kuwa yafaa mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, wala taifa zima lisiangamie.
Na neno hilo hakulisema kwa ajili yake mwenyewe;
Wala si kwa ajili ya taifa hilo tu, bali pia awakusanye watoto wa Mungu waliotawanyika wawe wamoja.
Basi tangu siku hiyo wakafanya shauri la kumwua.
Basi Yesu hakutembea tena hadharani kati ya Wayahudi; lakini alitoka hapo akaenda mpaka nchi iliyo karibu na jangwa, mpaka mji uitwao Efraimu, akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.
Sikukuu ya Pasaka ya Wayahudi ilikuwa karibu, na watu wengi kutoka mashambani wakapanda kwenda Yerusalemu kabla ya Pasaka ili kujitakasa.
Basi wakamtafuta Yesu, wakasemezana wao kwa wao wakiwa wamesimama Hekaluni, Mwaonaje?
Makuhani wakuu na Mafarisayo walikuwa wametoa amri kwamba mtu ye yote akijua aliko Yesu awajulishe ili wapate kumkamata.