Ikawa Yesu alipokuwa ameketi kula chakula nyumbani mwake, watoza ushuru wengi na wenye dhambi walikuwa wameketi pamoja na Yesu na wanafunzi wake; kwa maana walikuwa wengi wakamfuata.
Waandishi na Mafarisayo walipomwona akila pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi, wakawaambia wanafunzi wake, Mbona anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?
Yesu aliposikia akawaambia, Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio hawawezi. Sikuja kuwaita watu wema, bali wenye dhambi.
Wanafunzi wa Yohana na wa Mafarisayo walikuwa na desturi ya kufunga; wakaja na kumwambia, Mbona wanafunzi wa Yohana na wa Mafarisayo hufunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?
Yesu akawaambia, Je! maadamu wana bwana-arusi pamoja nao hawawezi kufunga.
Lakini siku zitakuja watakapoondolewa bwana-arusi, ndipo watakapofunga siku zile.
Hakuna mtu ashonaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kuukuu;
Wala hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu;
Ikawa siku ya sabato alipita katika mashamba ya ngano; wanafunzi wake wakaanza kwenda kukwanyua masuke.
Mafarisayo wakamwambia, Tazama, mbona wanafanya jambo lisilo halali siku ya sabato?
Akawaambia, Hamkusoma alivyofanya Daudi, alipokuwa na njaa, yeye na wale waliokuwa pamoja naye?
Jinsi alivyoingia katika nyumba ya Mungu siku za Abiathari, kuhani mkuu, akaila ile mikate ya wonyesho, ambayo hairuhusiwi kuliwa ila makuhani, akawapa na wale waliokuwa pamoja naye?
Akawaambia, Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, si mwanadamu kwa ajili ya sabato;
Kwa hiyo Mwana wa Adamu ndiye Bwana wa sabato pia.