Kitabu cha Kwanza cha Wakorintho, Biblia ya Sauti Bila Malipo, Biblia ya King James Version katika Kiswahili
Biblia ya King James Version
1 Wakorintho, Sura ya 13:
Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao.
Tena nijapokuwa na kipaji cha unabii, na kuelewa siri zote na maarifa yote; na nijapokuwa na imani yote, hata naweza kuhamisha milima, kama sina upendo, mimi si kitu.
Tena nijapotoa mali yangu yote kuwalisha maskini, tena nikitoa mwili wangu uchomwe, kama sina upendo, hainifai kitu.